HUYU MLINZI KINDA HATARI WA REAL KIDS, JANA KAKABA ULINZI TAIFA NOWMA, SAMIR AMPA TANO

Zanzibar ni Visiwa vyenye vipaji vingi sana ambapo kila siku vinaibuka vyengine vipya, tukija kwenye soka sitaki kuongea sana lakini jana kama umeangalia mchezo wa kirafiki kati ya Taifa ya Jang’ombe dhidi ya Gulioni katika uwanja wa Amaan, bila ya shaka umemuona kinda jipya limefunga mlango kwenye safu ya ulinzi ya Taifa, si mwengine bali ni Ibrahim Abdallah ni beki wa kati wa timu ya Real Kids inayoshiriki ligi za madaraja ya vijana wilaya ya Mjini, lakini jana alitumiwa na Taifa na alivaa jezi nambari 29 mgongoni.

Ibrahim unaweza ukamuona ni mlinzi wa kawaida lakini huyu dogo ni nowma hata Samir Yahya beki wa kati wa Taifa ya Jang’ombe amekubali kazi yake jana na kusema huyu mtoto hatari.

“Nime enjoy sana leo kucheza na Ibra katikati, dogo ana kibaji na anauwezo, anakuja vizuri sana naamini akizidi kucheza atakuwa bonge la beki hapa Zanzibar, nimefurahi sana na huwenda akawa mrithi wa Ninja au hata mimi nikiondoka basi naamini dogo ataziba pengo bila ya wasi wasi, kuna vitu vidogo tu vinarekebishika”. Alisema Samir beki wa Taifa.

Lakini yote 9, kumi wale walopata fursa ya kuangalia Mashindano ya Michezo na Sanaa ya Skuli za Sekondari Tanzania (UMISSETA), mashindano ambayo yalimalizika hivi karibuni katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Butimba huko mkoani Mwanza unaambiwa beki huyo alikuwa gumzo sana huko Mwanza, kama ulisikia Timu ya Unguja ilicheza zaidi ya mechi 4 bila ya kuruhusu kufungwa hata bao 1, basi kazi ya mlinzi huyo ilitendeka.

Mlinzi huyo yupo kwenye majaribio ya mwisho kujiunga na Taifa ya Jang’ombe ili kuziba pengo la Abdallah Haji Shaibu “Ninja” aliyesajiliwa Yanga pamoja na kuziba nafasi ya Ali Juma Maarifa “Mabata” ambae anatarajiwa kwenda Mkoani Manyara katika Mashindano ya Rolling Stone baada ya kuitwa kwenye Kombain ya Mjini Unguja.

Mtandao huu unamtakia kila la kheir mlinzi huyo Ibrahim Mungu amlinde kipaji chake.

Ibrahim Abdallah (Kushoto) na Samir Yahya (Kulia)

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS