GULIONI WANAKUJA KIVYENGINE MSIMU HUU, KWANZA WANAANZA NA TAIFA KISHA BOYS

Timu ya Soka ya Gulioni FC inayoshiriki ligi daraja la Pili Wilaya ya Mjini imepania kuwatia michezo miwili ya kirafiki kwenye sherehe za Sikuu ya Eid pili na nne ambapo Eid Pili watasukumana na Taifa ya Jang’ombe kisha Eid nne kucheza na Jang’ombe boys mechi zote zitachezwa saa 2:00 za usiku katika Uwanja wa Amaan.

Akizungumza na Mtandao huu Rais wa Gulioni Ahmed Khamis amesema maandalizi ya michezo hiyo yanaendelea vizuri na lengo lao ni kufanya mapinduzi ya soka la Zanzibar.


“Tumejiandaa vizuri kucheza na Taifa Eid pili kisha Boys Eid nne lakini sisi lengo letu ni kuleta mapinduzi ya soka la Zanzibar”. Alisema Ahmed.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS