GULIONI YAANZA MAANDALIZI MAPEMA MSIMU MPYA, SIKUKUU YA IDDI KUCHEZA NA TAIFA YA JANG’OMBE

Kikosi cha Gulioni msimu ulopita 2016-2017
Timu ya Gulioni itaanza rasmi mazoezi siku ya Jumatatu ya June 12, 2017 kwa kujiandaa na msimu wa ligi Daraja la Pili Wilaya ya Mjini wa mwaka 2017/2018.

Akizungumza na Mtandao huu Rais wa klabu ya Gulioni Ahmed Khamis amesema wamepania kuanza mapema mazoezi ili msimu huu wajipange kupandisha daraja timu yao.

Mbali na kuanza mazoezi hayo, Ahmed amesema pia wanatarajia kucheza michezo mbali mbali ya kirafiki ukiwemo mchezo wao dhidi ya Taifa ya Jang’ombe katika Bonanza maalum ambalo litafanyika katika sherehe za Sikukuu ya Iddi Pili katika Uwanja wa Amaan.

“Tunatarajia kuanza mazoezi Jumatatu, tunaanza mapema kwasababu tujiandae zaidi kuipandisha timu yetu, pia tutacheza na Taifa ya Jang’ombe Iddi Pili kwenye Bonanza maalum”. Alisema Ahmed.


Msimu ulopita wa mwaka 2016-2017 Gulioni ilifanikiwa kutinga katika hatua ya 4 bora ya Ligi daraja la Pili Wilaya hiyo lakini walishindwa kusonga mbele na kulazimika kusalia katika daraja la Pili Wilaya ya Mjini.
Wachezaji wa Gulioni wa msimu ulopita 2016-2017

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE