JANG’OMBE BOYS HAO DAR KUWAFATA GOR MAHIA YA KENYA KWENYE SPORT PESA CUP

Timu pekee ya Zanzibar iliyopata nafasi ya kushiriki Mashindano ya Sport Pesa Cup, Jang’ombe Boys wataondoka Visiwani Zanzibar kesho majira ya saa 3 za asubuhi kuelekea Jijini Dar es salam tayari kwa mchezo dhidi ya Gor mahia ya nchini Kenya mchezo ambao unatarajiwa kupigwa Jumanne ya June 6, 2017 saa 10:00 za jioni katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salam.

Kombe hilo ni la mtoano linashirikisha jumla ya timu nane , 4 kutoka Kenya, 3 Tanzania bara na 1 kutoka Visiwani Zanzibar.

RATIBA KAMILI HIYO
Jumatatu 5/6/2017
Singida united Vs FC leopard
Yanga Vs Tusker fc

Jumanne 6/6/2017
Simba Vs Nakuru All Star
Jang`ombe boys vs Gor mahia


Nusu fainali Alhamis 8/6/2017

Bingwa wa mechi kati ya Singida united vs AFC leopard atacheza na bingwa kati ya Yanga na Tusker.

Nusu fainali ya pili Bingwa wa mechi kati ya Simba na Nakuru all-star atacheza na bingwa wa mechi kati ya Jangombe boyz na Gor mahia



Fainali ni tarehe 11/6/2017 ambapo Bingwa wa SportPesa Super Cup ataondoka na kitita cha dola 30,000 huku mshindi wa pili akipata dola 10,000.
Jang'ombe Boys

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE