MAJERUHI YAIANDAMA UNGUJA, NYOTA WA 5 WA KIKOSI CHA KWANZA HUENDA WAKAIKOSA ROBO FAINALI LEO UMISSETA CUP

Kikosi cha Unguja
Timu ya Unguja inayoteremka Dimbani leo jioni kuwavaa wenyeji Mwanza katika uwanja wa Chuo cha Ualimu Butimba Mkoani Mwanza kwenye mashindano ya UMISSETA hatua ya robo fainali, imefikisha majeruhi 5 wa kikosi cha kwanza ambao ni Mlinzi Abdul Azizi Ameir, viungo Haji Suleiman na Iliyasa Suleiman, na washambuliaji Faki Kombo pamoja na Ibrahim Faraj “Mess”.

Wachezaji hao ambao ni nguzo kwenye kikosi hicho wana asilimia kubwa kukosa mchezo huo baada ya kupata majeraha katika michezo yao ya hatua ya makundi ikiwemo miwili ya jana ambapo mmoja walicheza asubuhi wakaipiga Iringa 2-1 na mwengine walicheza jioni wakatoka sare na Dar es salam 2-2.

Kocha Mkuu wa kikosi hicho Mohammed Ally Hilaly “Tedy” amekiri kuwa na majeruhi hao lakini bado anaimani timu yake itaibuka na ushindi leo.


“Ni majeruhi ambao ndio nguzo katika timu, lakini bado naimani ntashinda tu, ila Wazanzibar wajuwe kuwa mashindano hayo makugu sana, mana leo tunacheza robo, tukishinda kesho tutacheza nusu nap engine kesho kesho tutacheza fainali”. Alisema Tedy.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE