MAKOCHA WATAKIWA KUJIUNGA NA ZAFCA, NI BAADA YA ZFA KUPATA UANACHAMA WA CAF

Mustafa Hassan katibu msaidizi ZAFCA

Makocha wa soka Visiwani Zanzibar wametakiwa kwenda kujiunga na Chama cha Makocha “ZAFCA” ili kuzidi kuendeleza taaluma yao ya ukocha kwa kupata fursa mbali mbali zikiwemo kozi za makocha.

Kauli hiyo ameitoa katibu msaidizi wa ZAFCA Mustafa Hassan wakati anazungumza na Mtandao huu kwa kuwataka makocha waende wakajiunge na chama chao.

Amesema baada ya Zanzibar kupata uanachama wa 55 wa Shirikisho la Soka Barani Afrika “CAF” wamepokea mabadiliko na wametakiwa makocha wote wajiunge na chama chao ili watambuliwe na ZFA.

“Nawaomba makocha wenzangu waje kujiunga na ZAFCA, mana huko tunakokwenda ni kugumu mno, baada ya ZFA kuwa mwanachama wa CAF, tumetakiwa makocha wote wajinge na chama chao ili watambuliwe na ZFA na hapo ndipo utapata fursa ya kusoma kozi mbali mbali za makocha”. Alisema Mustafa.

Chama hicho cha makocha Zanzibar wanakutana kila siku ya Jumamosi katika darasa la Shule ya Sekondari ya Haile Selassie kuanzia saa 4:00 za asubuhi hadi saa 6:30 za mchana, hivyo kwa kocha yeyote anaetaka kujiunga na chama hicho afike hapo Haile kwa siku hiyo au amtafute kocha Nassor Salum wa Polisi au kocha Ibrahim Makeresa kwa kupatiwa fomu ya kujinga na uanachama ambayo inauzwa shilingi elfu mbili tu.



Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE