PEMBA SOKA WAMALIZA MECHI ZAO UMISSETA, WATOLEWA KATIKA MAKUNDI LAKINI WAMEMALIZA MECHI KWA FURAHA YA USHINDI

Kikosi cha Pemba

Timu ya Soka ya Pemba leo imemaliza michezo yake yote ya kundi “A” kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Tabora katika uwanja wa Chuo cha Ualimu Butimba Mkoani Mwanza kwenye mashindano ya UMISSETA.

Katika kundi lao hilo “A” walikuwa pamoja na timu ya Manyara, Simiyu, Arusha, Mwanza, Kigoma na Tabora ambapo wamecheza michezo 6 kwa kushinda mechi 2, sare 1 na kufungwa 3 wakijikusanyia alama 7.

Wenzao Unguja bado ni kinara wa kundi “C” wakiwa na alama 15, wakifukuzwa na Dar es salam wenye alama 13 wote wameshacheza michezo 5 na lakini timu zote hizo mbili zimeshakata tiketi ya kucheza hatua ya robo fainali.

Katika kundi hilo la Unguja lenye jumla ya timu 7 ambapo wapo pamoja na Katavi, Kagera, Mara, Mbeya, Iringa na Dar es salam.


Michezo mitano ya awali Unguja waliifunga Katavi 4-0, wakaichapa Kagera 3-0, juzi wakaipiga Mara 5-0, jana waituguwa Mbeya 1-0, na leo wakaipiga Iringa 2-1, hivyo wameshafunga jumla ya mabao 15 katika michezo 5 waliyocheza wakati lango lao limeruhusu kufungwa bao moja tu.
Kikosi cha Unguja

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE