UMISSETA ZANZIBAR WAMEREJEA NYUMBANI NA VIKOMBE 4

Zaidi ya Wanamichezo 134 kutoka Unguja na Pemba wamerejea Visiwani Zanzibar mchana wa leo Jumamosi June 17, 2017 wakitokea Butimba Mkoani Mwanza, kushiriki mashindano ya umoja wa Michezo na Sanaa skuli za sekondari Tanzania (UMISSETA).

Akizungumza na Wanamichezo hao Bandarini Malindi Mjini Unguja Naibu waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mmanga Mjengo Mjawiri amewapongeza kwa kushindana katika mashindano hayo baada ya kurejea na vikombe 4, moja cha mshindi wa kwanza na vitatu vya mshindi wa tatu.

“Kwa niaba ya Wizara ya Elimu Zanzibar nakupongezeni sana kwa ushiriki wenu wa michezo kule Mwanza,  na pia nakupeni hongereni kwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu, sisi Wizara tutaendelea na kuvitunza vipaji Mashuleni”. Alisema Mjawiri.

Mashindano hayo yaliyoanza June 6 na kumalizika juzi June 15, 2017 katika Viwanja vya Chuo cha Ualimu Butimba Mkoani Mwanza ambapo Zanzibar walifanikiwa kushinda nafasi ya kwanza kwa Wanaume kwenye mbio za Relay Mita 100 x 4, wakati kwa Mpira wa Kikapu, Wavu na mpira wa Mikono yote wakishika nafasi ya 3.
  
Hassan Tawakal Khairallah (wa kati kati) Mkurugenzi wa Idara ya Michezo na Utamaduni katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar akimkabidhi kombe Naibu waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mmanga Mjengo Mjawiri 



Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE