CAPTAIN WA GULIONI AWA MZANZIBAR MWENGINE KUSAJILIWA LIGI KUU BARA

Timu ya Stand United kutoka mkoani Shinyanga imemsajili beki wa kati ambae ni nahodha wa timu ya Gulioni Ali Hamad Ali “Kinibu” akitokea kwenye ligi daraja la pili wilaya ya mjini Unguja.

Kinibu amesajiliwa kwenye kikosi hicho cha wapiga debe wa Shinyanga kwaajili ya kuongeza nguvu msimu ujao wa mashindano yakiwemo kombe la FA pamoja na ligi kuu soka Tanzania bara.

Mara baada ya kusaini miaka 2 kuitumikia timu hiyo Kinibu amefurahishwa mno na kusema malengo yake ni kucheza nje ya Tanzania hivyo ataendelea kupambana  ili atimize ndoto zake.

“Nimefurahi kusaini mkataba wa miaka 2 Stand United, malengo yangu ni kucheza nje ya Tanzania ntaendelea kujituma ili nitimize ndoto zangu”. Alisema Kinibu.


Kinibu anavutiwa zaidi na uchezaji wa mlinzi wa kati wa klabu ya Arsenal na timu ya Taifa ya Ufaransa Laurent Koscielny pamoja na mlinzi wa Spain Sergio Ramos.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS