FC MUEMBE BENI WAANZA VYEMA KUTETEA TAJI LAO CENTRAL LIGI, REAL KIDS HOI KWA SCHALKE 0

FC Muembe Beni

Mabingwa watetezi wa ligi za madaraja ya Vijana ndani ya Wilaya ya Mjini kwa upande wa daraja la Central timu ya FC Muembe beni imeanza vyema kampeni zake za kutetea taji lao baada ya kuifunga King Boys mabao 2-0 kwenye mchezo wa 4 bora uliopigwa leo Jumapili July 9, 2017 kwenye dimba la Amaan saa 5 za asubuhi.

Mabao ya Muembe beni yamefungwa na Mselem Ali dakika 15 na Othman Arafat dakika ya 89.

Mchezo mwengine umepigwa majira ya saa 7 za mchana ambapo Real Kids watoto wa Kikwajuni wakafundishwa soka na watoto wa Muembe Makumbi ambao ni Schalke 04 baada ya kufungwa mabao 2-1.


Mabao ya Schalke 04 yamefungwa na Iliyasa Suleiman dakika 6 na 18 wakati bao pekee la Real Kids limefungwa na Abdul halim Mohd dakika ya 39.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE