JKU NA ZIMAMOTO HAKUNA MBABE, JAMHURI YAPATA USHINDI MNENE, KESHO TAIFA NA BOYS


Mzunguko wa 9 wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora umeanza jioni ya leo kwa kupigwa michezo 2 katika viwanja 2 tofauti.

Katika uwanja wa Amaan kisiwani Unguja timu ya JKU na Zimamoto wameshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya 1-1.

Bao la Zimamoto limefungwa na Ibrahim Hamad Hilika dakika ya 15 wakati bao la JKU limefungwa na Is haka Othman “Bopa” dakika ya 81.

Nako huko katika uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba, timu ya Jamhuri imeondoka na alama 3 muhimu baada ya kushinda mabao 5-3 dhidi ya Mwenge.

Mabao ya Jamhuri yamefungwa na Mwalimu Mohammed (Hat trick) dakika ya 11, 15, 27, Khamis Abrahman “Mburu” dakika ya 60, na Mussa Ali Mbarouk dakika ya 88 ambapo mabao ya Mwenge yote matatu (Hat trick) yamefungwa na Abdull Yussuf dakika ya 33, 37 na 79.


Ligi hiyo itaendelea tena kesho saa 10:00 za jioni kwa kupigwa mchezo kati ya Taifa ya Jang’ombe dhidi ya Jang’ombe Boys kwenye uwanja wa Amaan na katika uwanja wa Gombani watasukumana kati ya Okapi dhidi ya Kizimbani.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS