KAMATI YA SOKA LA UFUKWENI ZANZIBAR KUANDAA MASHINDANO YA KLABU BINGWA YA AFRIKA MASHARIKI

Kamati ya soka la ufukweni visiwani Zanzibar imevialika vilabu vitatu kutoka Uganda kwaajili ya kucheza Mashindano ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki ya Beach Soka Mashindano ambayo yanatarajia kuanza rasmi 4/9/2017 katika Fukwe za Bububu Bambuu Visiwani hapa.

Akizungumza na Mtandao huu Rais wa Beach Soka Visiwani Zanzibar Ali Sharifu “Adolf” amesema kwa vile Afrika Mashariki nzima nchi zenye ligi kuu ya Beach soka ni wao Zanzibar na Uganda tu ambapo nchini nyengine hawana ligi hiyo ndio mana wakavialika vilabu vya Uganda vitatu na vya Zanzibar vitatu kisha watacheza Mashindano hayo.

“Unajua kwa Afrika Mashariki nzima Zanzibar na Uganda pekeyetu ndo tunaocheza ligi kuu ya Beach soka, nchi nyengine hawana ligi kuu labda mabonanza tu na timu zao za Taifa, lakini nchi mbili hizi ndo zinazocheza ndo mana tumevialika vilabu vya Uganda kucheza na Zanzibar kwaajili ya kumtafuta Bingwa wa Beach Soka Afrika Mashariki nzima”. Alisema Adolf.


 Timu 6 zitakazoshiriki katika Mashindano hayo ni Malindi, Green River na Lavister kutoka Zanzibar na kutoka Uganda ni Makerere University, Mutesa 1 Royal University na St. Laurence University.

 
Viongozi wakuu wa Kamati ya Soka la Ufukweni Zanzibar

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE