KESHO NDIO KESHO KUJUA MFUMO UPI WA KUPATIKANA TIMU 12 ZA LIGI KUU MSIMU MPYA 2017-2018 UTAJULIKANA

Baadhi ya wajumbe wa Vilabu vya Soka Unguja wamesafiri kwa Meli ya MV Mapinduzi asubuhi ya leo kwenda kisiwani Pemba katika kikao maalum cha  Vilabu 28 ambavyo vimo katika mchakato wa upatikanaji wa timu 12 za ligi kuu soka ya Zanzibar msimu mpya wa mwaka 2017-2018 ambapo watakutana na kupanga mchakato mzima wa upatikanaji wa timu kumi na mbili za ligi kuu msimu wa 2017-2018, kikao ambacho kitafanyika kesho Jumamosi ya July 8, 2017 saa 3:00 za asubuhi katika Ukumbi wa Mikutano wa uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba.

Hayo yote yamekuja baada ya ZFA kuwa mwanachama wa 55 wa Shirikisho la Soka Barani Afrika “CAF” ambapo moja ya agizo lao CAF ni kutaka msimu ujao wa mwaka 2017-2018 ligi kuu soka ya Zanzibar iwe na jumla ya timu 12 kwa Zanzibar nzima ambapo katika msimu huo wa mwaka 2016-2017 ulikuwa na jumla ya timu 36 kwa kila kanda ilikuwa ina timu 18, yani Kanda ya Unguja 18 na Kanda ya Pemba 18, huku zimeshashuka timu 12 kati ya hizo 36 kwa kila kanda zimeshuka timu sita (6).


Viongozi wawili wawili wa Timu 14 za Unguja wanaohitajika Pemba katika Mkutano huo ni kutoka JKU, Zimamoto, Jang’ombe Boys, Taifa ya Jang’ombe, Mafunzo, KMKM, Black Sailors, Polisi, Chuoni, Kipanga, Kilimani City,KVZ , Miembeni City na Charawe ambapo watashirikiana na vile vilabu 14 vya Pemba ili kupanga  mchakato mzima wa upatikanaji wa timu kumi na mbili za ligi kuu msimu wa 2017-2018.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE