KIPWIDA CUP KUANZA JUMAMOSI, HII HAPA RATIBA NA MAKUNDI

Abdul rahim Kipwida
Mashindano ya Ndondo ya KIPWIDA CUP yanatarajia kuanza rasmi Jumamosi July 8, 2017 kwenye uwanja wa Lion kids huko Maungani ambapo watazindua kati ya Big Nation dhidi ya Kisaka saka saa 10:00 za jioni.

Akizungumzia matayarisho ya Mashindano hayo mratibu Abdul Rahim Kipwida amesema maandalizi ya mashindano hayo yanaendelea vizuri ambapo mwaka huu Bingwa atapatiwa Zawadi ya Ng’ombe huku mshindi wa pili atazawadiwa Mbuzi Mnyama.

“Maandalizi yamekamilika tunasubiri ifike Jumamosi tu, mwaka huu Bingwa atapata Ng’ombe na wa pili tutampatia Mbuzi, lakini zawadi zitaongezeka zaidi ya hizo”. Alisema Kipwida.

Katika Mashindano hayo mwaka huu kuna makundi manne (4), kundi “A”, “B”, “C” na “D”.

KUNDI “A”
Big Nation, Kisaka saka, Basra Boys na Mpira Pesa

KUNDI “B”
African Sports, Lakidatu, Red Scorpion na Kisaka saka Boys

KUNDI “C”
Lion Kids, Umoja Star, Njaa Kali na Polisi Mazizini

KUNDI “D”
Chilla All Star, Mtoko Pensi, Top Life na New Manter.

RATIBA YA MZUNGUKO WA KWANZA
Jumamosi July 8, 2017 Big Nation v/s Kisaka saka
Jumapili July 9, 2017 Basra Boys v/s Mpira pesa
Jumatatu July 10, 2017 African Sports v/s Lakidatu
Jumanne July 11, 2017 Red Scorpion v/s Kisaka saka Boys
Jumatano July 12, 2017 Lion Kida v/s Umoja Star
Alhamis July 13, 2017 Njaa kali v/s Polisi Mazizini
Ijumaa July 14, 2017 Chilla All Star v/s Mtoko Pensi

Jumamosi July 15, 2017 Top life v/s New Manter

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE