KOCHA KIDUU MWENYE LESENI “A” LICHA YA KUONGOZA LIGI YA ZENJ BADO AKIRI KUWA NGUMU

Kocha Mkuu wa timu ya Jamhuri, Abdul mutik Haji (Kiduu), amekiri ligi kuu ya Zanzibar hatua ya 8 bora ni ngumu na kwamba hadi sasa na hakuna timu ambayo imejihakikishia kutwaa ubingwa wa ligi hiyo inayofikia tamati Jumapili ya 20/8/2017.

Kiduu amesema licha ya timu yake kuongoza lakini bado ligi mbichi na timu zote 8 zina nafasi lakini atapigana kuhakikisha timu yake inaendelea kuongoza hadi mwisho wa ligi hiyo.

“Bado ligi ni ngumu mno, timu yoyote ina nafasi ya kutwaa ubingwa, mimi kubwa ntahakikisha naendelea kuongoza mpaka mwisho”. Alisema Kiduu.

Jamhuri ndie kinara wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora akiwa na alama 12 akipata ushindi michezo yote 4 baada ya awali kuwafunga Mwenge mabao 3-2, kisha kuwachapa Okapi 3-0, wakaendelea kuwapiga Kizimbani 3-0 na juzi tu wakawamaliza Zimamoto kwa mabao 2-1.


Jamhuri watashuka tena Dimbani Ijumaa ya July 14, 2017 dhidi ya Taifa ya Jang’ombe saa 10 za jioni katika uwanja wa Amaan.
Kocha Abdul mutik Haji (Kiduu)

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE