MAKAMO WA RAIS ZFA AFUNGUA KOZI YA MAKOCHA WA MAKIPA ZANZIBAR

Makamo wa Rais ZFA Unguja Mzee Zam Ali leo saa 3:00 za asubuhi alikuwa Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa  Kozi ya awali ya makocha wa Magilikipa, kozi ambayo imeanza leo Jumatano  July 5 na kumalizika Jumanne July 11, 2017 chini ya Mkufunzi Gwiji  Saleh Ahmed Seif “Machupa”.

Kozi hiyo imeandaliwa na Chama cha Soka Zanzibar “ZFA” ambayo itawashirikisha zaidi ya makocha 30 kutoka Unguja na Pemba na makocha hao wakimaliza kozi hiyo watapata fursa ya kutambuliwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika “CAF”.


Machupa ni Mkufunzi pekee nchini Tanzania aliyehitimu Kozi ya CAF ya Wakufunzi wa Makocha wa Magolikipa wa ndani kozi ambayo aliisomea nchini Cameroon mwanzoni mwa mwezi Mei mwaka huu,  Machupa pia ameshahitimu kozi ya FIFA ya Ukocha wa Magolikipa ya hatua ya juu (Advanced Level) ambayo aliipata kwenye kozi iliyofayika tarehe 01 Agost, 2016 na kumalizika tarehe 05 Agost 2016, na pia Machupa ana Leseni “B” ya Ukocha inayotambuliwa na CAF.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE