MFUNGAJI WA JAMHURI KUKOSA MECHI ZOTE ZA JULY LIGI KUU YA ZANZIBAR

Mshambuliaji hatari wa klabu ya Jamhuri Khamis Abdulrahman Hamad “Mburu” atalazimika kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki tatu.

Nyota huyo atakaa nje ya uwanja kwa wiki tatu kufuatia kuchanika kwa nyama za paja la kushoto akiuguza jeraha hilo ambapo atakosa zaidi ya michezo 8 katika ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora.

Mburu ataanza kukosa michezo miwili yote timu yake itakayocheza Unguja katika Uwanja wa Amaan ukiwemo wa Jumatatu July 10 kati ya Zimamoto dhidi ya Jamhuri, na mwengine wa Alhamis July 13, 2017 kati ya Taifa ya Jang’ombe dhidi ya Jamhuri ambapo pia akitarajiwa kukosa na michezo mengine ambayo yote itakayochezwa mwezi July.

“Daktari amenambia nitakaa nje zaidi ya wiki 3, ila kwasasa naendelea vizuri afya yangu namshkuru Mwenyezi Mungu, mana paja langu la kushoto lilichanika sana juzi”. Alisema Mburu.


Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE