MJINI UNGUJA NA JKU CADEMY WAKISHINDA WOTE KESHO NUSU FAINALI, BASI WATAKUTANA FAINALI MASHINDANO YA ROLLING STONE

Kikosi cha Mjini Unguja cha jana kilichoshinda 5-1 robo fainali

Na: Kennedy Lucas na Said Salim “Hazard” kutoka Mbulu, Manyara.

Baada ya jana kushinda Wawakilishi wawili wote wa Zanzibar katika Mashindano ya vijana ya Afrika Mashariki na kati ya Rolling Stone timu ya Mjini Unguja na JKU Academy ambao wamefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali, sasa kesho wakifanikiwa kushinda katika michezo yao ya nusu fainali watakutana fainali Wazanzibar wawili hao.

Mjini Unguja jana walitinga nusu fainali baada ya kuitoa Lindi academy kwa mabao 5-1 huku magoli ya Mjini yalifungwa na Ibrahim Abdalla (Imu Mkoko )2, Mohamed Mussa (Modi) 2 na Mohamed Haji (X Box) 1.

JKU Academu wametinga hatua ya nusu fainali baada ya Arusha Center Academy ya Arusha kuondolewa Kwenye Mashindano hayo baada ya kuwachezesha wachezaji wanne ambao umri wao umezidi miaka 17 katika mchezo wao wa Robo fainali ya Mashindano hayo dhidi ya JKU mchezo ulipigwa katika uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid Kaluta Jijini Arusha Ambapo Arusha Center waliibuka na ushindi wa bao 1-0.

Baada ya mchezo kumalizika JKU walikata rufaa wakiilalamikia Arusha Center Kuwachezesha Wachezaji 3 ambao wanaumri zaidi Ya Miaka 17 ambayo hairuhusiwi kutokana na kanuni na taratibu zinavyo sema kwani Mchezaji anaeruhusiwa kucheza Mashindano hayo ni mwenye umri wa chini ya miaka 17.

Baada ya kuipitia rufaa hiyo Kamati Ya Mashindano ya Rolling Stone ikaamua kuiondosha katika Mashindano hayo timu Ya Arusha Center Academy kutokana na timu hiyo kuchezesha Wachezaji ambao hawaruhusiwi kucheza, hivyo JKU Academy Sasa wamepita kwa Rufaa hiyo.

Mapema kesho Jumapili saa 8:00 za mchana JKU Academy kutoka Zanzibar watasukumana na Fire Boys kutoka Karatu Arusha kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza.

Mabingwa watetezi timu ya Kombain ya Mjini kutoka Zanzibar watacheza nusu fainali ya pili dhidi ya Trust Saint Patrick Academy ya Arusha mchezo utapigwa saa 10:00 za jioni.

Michezo yote hiyo itapigwa katika uwanja wa Julias Nyerere Wilayani Mbulu Mkoani Manyara.

Jumatatu ya July 7, 2017 ni siku ya mapumziko ambapo Jumanne ya July 18, 2017 ni siku ya kutafuta Mshindi wa 3, 2 na Bingwa.


Mashindano ya Mpira wa Miguu kwa Vijana waliochini ya umri wa miaka 17 Afrika Mashariki na Kati maarufu kama Rolling Stone, Mwaka huu 2017 yanafanyika katika Mikoa Ya Arusha na Manyara huku Manyara wakipata fursa ya Kuandaa Mashindano Hayo Kwa Mara ya Kwanza na kupewa Vituo Vitatu Vya Mbulu,Babati na Mererani wakati changamoto kubwa katika Mashindano hayo yakiwa ni uchezeshwaji wa Wachezaji Wenye Umri Zaid Ya Miaka 17.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE