MKUFUNZI KUTOKA SWEDEN AWAPIGA MSASA TAEKWON-DO ZANZIBAR

Chama cha mchezo wa Taekwon-do visiwani Zanzibar, kimeandaa semina maalum ya siku moja kwa wachezaji wa mchezo huo ambapo mkufunzi wa mafunzo hayo ametoka nchini Sweden.

NIKLAS ENANDER ni mkufunzi anayetambulika na Shirikisho la Taekwon-do Duniani (ITF) ndie aliyeendesha Mafunzo hayo ya siku moja, Mafunzo ambayo yamefanyika Jana Amani mjini Unguja katika ukumbi wa Judo kuanzia saa 3:00 asubuhi na kumalizika saa 11:00 za jioni.


NIKLAS amefurahishwa sana kuona idadi ya wachezaji imezidi tofauti na mwaka jana alipokuja hivyo amezidi kupata moyo wa kuwa karibu na Wazanzibar.

“Nimefurahi sana kuona Wazanzibar wanapenda michezo, mwaka jana nilipokuja wachezaji walikuwa kidogo, lakini mwaka huu idadi imeongezeka, ukweli nimefurahi sana”. Alisema Mkufunzi huyo.

Mchezo wa Taekwon-do asili yake ni nchini Korea kwa lugha nyepesi unaweza ukauwita sanaa ya mapambano na pia unafanana na mchezo wa karati lakini ni tofauti kabisa licha ya kuwa mchezo huo pia wanatumia kupiga mateke na kurusha ngumi .

Mchezo huo unafundishwa katika ukumbi wa Judo Amani Mjini Zanzibar na kocha Maxmiliana Kailangana kwa kila siku ya Jumatatu, Jumatano na Alhamis kuanzia saa 1:00 usiku hadi 3:00 usiku huku kocha huyo akiwataka wadau wengine kujitokeza kushiriki mchezo huo.




Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE