MLANDEGE WAPANIA KUPANDA DARAJA, WAANZA KWA KISHINDO LEO

Timu ya Mlandege kutoka Wilaya ya Mjini imeanza vyema ligi ya mabingwa wa Daraja la Pili Wilaya baada ya jioni ya leo kuwafunga Azimio ya Wilaya ya Magharibi "B" mabao 3-0 mchezo uliosukumwa katika uwanja wa Amani.

Mabao ya Mlandege yamefungwa na Sajini Remtula dakika 15, Hassan Ramadhan dakika 31 na Omar Makame Makungu dakika ya 70.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa kupigwa mchezo mmoja katika uwanja wa Amaan kati ya Mapinduzi kutoka Wilaya ya Kusini watasukumana na New Power kutoka Wilaya ya Kati saa10 za jioni.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE