RAIS WA JANG’OMMBE BOYS AONYESHA MAKALI YAKE MPAKA PEMBA, BOYS WAKIIPIGA MWENGE, BAADAE ZAMU YA TAIFA

Mshambuliaji hatari wa timu ya Soka ya Jang’ombe Boys Khamis Mussa (Rais) ameendelea kuonyesha makali yake baada ya kufunga mabao yote mawili timu yake ilipoichapa Mwenge mabao 2-1 katika mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora uliosukumwa jioni ya leo katika uwanja wa Gombani.

Rais mabao hayo ameyafunga katika dakika ya 27 na 77 ambapo Mwenge walitangulia kupata bao lililofungwa na Ali Salim Bajaka dakika ya 18 ya mchezo huo.

Ligi hiyo itaendelea tena baadae saa 1 za usiku katika Uwanja wa Amaan kati ya Taifa ya Jang’ombe dhidi ya Kizimbani.

RATIBA YA MECHI ZA KESHO:-
10/7/017 Okapi vs JKU saa 10 alasiri uwanja wa Gombani

10/7/017 Zimamoto vs Jamhuri saa 10 alasiri uwanja wa Amaan

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE