TAIFA YA JANG’OMBE KAMA SHAMBA LA BIBI, KIZIMBANI AMEJICHULIA MATUNDA YAKE, KESHO HAPATOSHI ZIMAMOTO v/s JAMHURI

Kikosi cha Taifa ya Jang'ombe mwanzoni mwa msimu huu

Timu ya Taifa ya Jang’ombe imekubali kufungwa mabao 3-1 nyumbani kwao Unguja na timu ya Kizimbani kutoka Pemba katika mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora uliopigwa saa 1 usiku leo katika uwanja wa Amaan.

Mabao ya Kizimbani yamefungwa na Khatib Hassan dakika 11, Ali Othman Mussa dakika ya 72 na Nassir Suleiman dakika ya 90 wakati bao pekee la Taifa limefungwa na Ali Badru dakika 61.

Mapema hii leo Jang’ombe Boys wameichapa Mwenge 2-1 katika uwanja wa Gombani.

RATIBA YA MECHI ZA KESHO:-
10/7/017 Okapi vs JKU saa 10 alasiri uwanja wa Gombani

10/7/017 Zimamoto vs Jamhuri saa 10 alasiri uwanja wa Amaan

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE