TAIFA YAENDELEZA UTEJA KWA BOYS, YAPIGWA MARA 3 MFULULIZO

Timu ya Jang'ombe boys imeendeleza wimbi lake la ushindi mbele ya kaka zao Taifa ya Jang'ombe baada ya kushinda mabao 2-0 katika mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar uliopigwa jioni ya leo katika uwanja wa Amaan.

Mabao ya Boys yamefungwa na Hafidh Barik (Fii) dakika ya 6 na Juma Ali (Mess)  dakika ya 66.

Nako huko katika uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba timu ya Kizimbani wakaichapa Okapi mabao 2-1.

Mabao ya Kizimbani yamefungwa na Khamis Suleiman dakika ya 49 na Haji Rashid dakika 62 wakati bao pekee Okapi limefungwa na Seif Saleh dakika ya 90.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS