VIONGOZI WA ZFA WAWILI WANAWASILI LEO SAA 4 ASUBUHI WAKITOKEA RABAT MOROCCO WALIPOPOKONYWA UANACHAMA NA CAF
Ravia Idarous Faina Rais wa ZFA (Picha ya zamani baada ya ZFA kupewa ZFA) |
Rais wa Chama cha Soka Visiwani Zanzibar (ZFA) Ravia Idarous
Faina pamoja na kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) Hemed
Suleiman “Morocco” wanatarajiwa kuwasili Visiwani Zanzibar saa 4:5 asubuhi ya
leo Jumatatu ya July 24, 2017 kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid
Amani Karume.
Ravia na kocha Morocco wameondoka Nairobi nchini Kenya asubuhi
ya leo saa 1:35 na watatua Zanzibar asubuhi hii saa 4:05.
Katibu Mkuu wa ZFA Mohd Ali Hilali “Tedy” yeye ametua Cairo
nchini Misri saa 11:40 za alfajiri ya leo, kisha leo usiku saa 5 ataondoka
Cairo na atawasili Nairobi Kenya Alfajiri ya kesho saa 11 kisha ataondoka
Nairobi kesho saa 1:35 za asubuhi na atawasili Zanzibar saa 4:05 za asubuhi.
Viongozi hao wa ZFA walikuwepo katika Mkutano wa Shirikisho la
Soka Barani Afrika (CAF) chini ya Kamati ya utendaji wa Shirikisho hilo ambao ulikutana
mjini Rabat, Morocco na kuamua mambo kadhaa likiwemo hilo la Zanzibar kufutiwa
uanachama ambapo Wazanzibar wengi pamoja na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar wanasubiri ripoti ya Viongozi hao ili kujulikana kwa kina mpaka
Zanzibar wakavuliwa uanachama kisha Serikali watatoa taarifa rasmi baada ya
kupewa ripoti hiyo na ZFA huku Serikali ikiwasisitiza Wananchi kuwa na
uvumilivu na subira katika kipindi hichi.
Ijumaa iliyopita Rais wa Caf, Ahmad Ahman alisema Zanzibar
ilipewa nafasi hiyo kimakosa na si sahihi kwa nchi moja kuwa na wanachama
wawili wa shirikisho hilo.
Zanzibar ilipewa uanachama wakati wa utawala wa Issa Hayatou
ambaye alikuwa akiungwa mkono na TFF chini ya Jamal Malinzi, hata hivyo Hayatou
aliangushwa na Ahmad Ahmad ambaye aliibuka mshindi katika uchaguzi wa CAF.
Siku ya Alhamis Machi 16, 2017 itaendelea kukumbukwa na
Wazanzibar baada ya ZFA kuingizwa rasmi kuwa Mwanachama wa 55 wa Shirikisho la
Soka Barani Afrika “CAF” kufuatia Kikao cha 39 cha Mkutano Mkuu wa Shirikisho
hilo kilichofanyika Addis Ababa nchini Ethiopia, uanachama huo umedumu kwa siku
128 tangu siku hiyo mpaka Ijumaa July 21, 2017.
Katika kura 54 za CAF, kura 51 zimekubali Zanzibar ipatiwe
uanachama wa kudumu wa Shirikisho hilo na nchi 3 zilikataa Zanzibar isipatiwe
ambazo ni Madagascar, Benin na Seychelles ambapo Madagascar ndio nchi anayotoka
Rais wa sasa wa CAF Ahmad Ahmad.
Ypulchtechpecgu Tim Gray https://wakelet.com/wake/iU7cNjcmWRN13wSHOtgDP
ReplyDeletetamdroogahve
cipernet-nu Tonya Brown This is there
ReplyDeleteDownload
seturedro