WANAMICHEZO WAPATA SHAVU, WATEULIWA KUWA MASHEHA, MMOJA KATIBU WA WAAMUZI, MUAMUZI, MSHIKA FEDHA NA ALOKUWA KATIBU WA SQUASH

Haji Uzia Vuai kuwa Sheha wa Shehia ya Mikarafuuni 
Jumanne iliyopita ya July 4, 2017 Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohammed Mahmoud alifanya uteuzi wa masheha wapya wa shehia takriban 120 za mkoa huo.

Masheha walioteuliwa siku hiyo wamo wanamichezo nguli Visiwani Zanzibar miongoni mwao ni Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi ZFA Taifa Issa Ahmada Hijja “Jogoo” ambae ameteuliwa kuwa Sheha wa Shehia ya Mtopepo Wilaya ya Magharibi “A” Unguja.
 
Ali Haji Ali “Mkenya”  Sheha wa Shehia ya Kwa Goa akiapa mbele ya mkuu wa Mkoa
Mwengine ni Muamuzi wa Soka wa ZFA Taifa ambae ni Ali Haji Ali “Mkenya” ambapo ameteuliwa kuwa Sheha wa Shehia ya Kwa Goa Wilaya ya Magharibi “A” Unguja.

Aidha Mkuu wa Mkoa huyo pia alimteuwa mwana michezo mwengine aliyekuwa katibu wa chama cha mpira wa Ukuta Zanzibar (Squach) ambae ni Haji Uzia Vuai kuwa Sheha wa Shehia ya Mikarafuuni Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.

Mwengine aliyeteuliwa kuwa Sheha ni Mshika Fedha wa ZFA Wilaya ya Magharibi “B” Khamis Mzee Mwinshehe “Bonzo” kuwa Sheha wa Shehia ya Maungani.

Tayari viongozi hao jana wameshaapishwa mbele ya Mkuu wa Mkoa wao ili kuzitumikia nafasi zao.
Issa Ahmada Hijja Sheha wa Shehia ya Mtopepo

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE