WATATU WAFUKAZANA KWA KUPACHIKA MABAO LIGI KUU YA SOKA ZANZIBAR

Mshambuliaji wa timu ya Jang’ombe Boys Khamis Mussa “Rais”, Ahmed Ali wa Jamhuri pamoja na Mwalimu Mohd wa Jamhuri wao ndio vinara wa kupachika mabao kwenye ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora inayoendelea katika mzunguko wake wa sita.

Washambuliaji hao mpaka sasa wameshafunga jumla ya mabao 4 kila mmoja katika michezo mitano waliyocheza.

Wengine wanaofuatia ni Ibrahim Hamad  “Hilika”  wa Zimamoto, Khamis Said wa JKU, Nassor Matar wa JKU, Nabil Mohammed wa Okapi, Seif Saleh wa Okapi, Abdull Yussuf wa Mwenge, Salim Mussa wa Mwenge, Khatib Hassan wa Kizimbani, Nassir Suleiman wa Kizimbani, Mussa Ali wa Jamhuri na Hassan Haji wa Zimamoto wote hao wana mabao 2.


Hakim Khamis “Men” ndie Mfungaji bora wa ligi kuu soka ya Zanzibar msimu ulopita alifunga mabao 17 na kuisaidia timu yake Zimamoto kutwaa ubingwa wa ligi hiyo ambapo pia aliwahi kuwa mfungaji bora wa ligi kuu soka ya Zanzibar msimu wa mwaka 2011-2012 wakati Super Falcon ya Pemba ilitwaa ubingwa msimu huo.
Khamis Mussa (Rais) mshambuliaji wa J Boys

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE