YULE MCHEZAJI WA MAFUNZO ALIYECHOMWA KISU NA KUKOSA KUCHEZA SOKA MWAKA MZIMA SASA YUPO FITI NA AMESHAANZA MAZOEZI NA WENZAKE

Mlinzi wa Kati wa timu ya Soka ya Mafunzo Kheri Salum Kheri “Chivu” amerejea mazoezi katika kikosi chake na kuanza kujifua na wenzake baada ya kukosa Mwaka mzima.

Beki huyo amerudi uwanjani baada ya kukaa nje msimu mzima uliopita wa mwaka 2016-2017 ambapo alipata tatizo kufuatia kuchomwa kisu na kijana mmoja anatuhumiwa kuwa ni muhalifu huko nyumbani kwao Migombani Mjini Unguja ambapo tukio hilo lilitokea karibu ya mwaka sasa, na awali alianza kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Mnazi mmoja kisha kufanyiwa upasuaji katika Hospitali ya Kairuki na Muhimbili huko Tanzania bara.

“Narudi uwanjani katika kipindi muhimu ambacho timu inanihitaji kutokana na ugumu wa ligi 2, kama unavyojua sasa kuna ligi 1 na 2 na sisi Mafunzo tupo ligi 2 hivyo nataka kupigana tuipeleke Mafunzo ligi 1, wenzangu wamenimis sana mwaka mzima lakini kwasasa namshukuru Mwenyezi Mungu nimepoa na mazoezi nimeshaanza na wenzangu”.  Alisema Kheri.

Kheri ni kaka wa damu wa Abdallah Salum Kheri (Sebo) Beki wa Azam FC na Omar Salum Kheri “Inzaghi” mlinzi wa kushoto wa African Lyon ndugu zake wote wakicheza soka Tanzania bara.

 
Kheri Salum Kheri “Chivu”  wa kushoto

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE