ZANZIBAR IMEONJESHWA HARUFU YA CAF KWA SIKU 128, SASA RASMI YAVULIWA UANACHAMA

Ni taarifa mbaya kwa soka la Zanzibar baada ya kuwa mwanachama wa 55 wa Shirikisho la Soka Barani Afrika kwa siku 128, sasa rasmi Zanzibar imevuliwa uanachama huo.
  
Raisi wa Shirikisho hilo Ahmad Ahmad amesema Zanzibar walipewa uanachama kimakosa na kama sheria zingepitiwa vizuri wasingepewa uanachama ambapo Sababu kubwa ambayo CAF wameivua uanachama Zanzibar ni kutokana na Visiwa hivyo kuwa ndani ya Tanzania ambao nao ni wanachama wa CAF..

“Walipewa uanachama bila kupitia vizuri kanuni ambazo ziko wazi na zinaeleza kila kitu, kama kanuni na sheria zingepitiwa kiufasaha wasingepewa uanachama”

“Jina la nchi linatokana na jina linaloandikwa katika umoja wa mataifa UN na Zanzibar katika umoja huo inafahamika ipo ndani ya nchi iitwayo Tanzania ambao ni wanachama wa CAF”. Alisema Ahmad.

Machi 16, 2017 ilikuwa ni siku nzuri na yenye historia kubwa kwa Zanzibar baada ya kuingizwa rasmi kuwa Mwanachama wa 55 wa Shirikisho la Soka Barani Afrika “CAF” kufuatia Kikao cha 39 cha Mkutano Mkuu wa Shirikisho hilo kilichofanyika Addis Ababa nchini Ethiopia lakini leo July 21, 2017 ni siku mbaya kwa Zanzibar baada ya kuvuliwa rasmi uanachama huo.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE