ZASWA KUFANYA UHAKIKI HUKU WAKIJITAYARISHA NA UCHAGUZI, WAANDISHI WA MICHEZO WAHIMIZWA WAJIUNGE NA CHAMA HICHO

Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Zanzibar (ZASWA) kinatarajia kufanya Uchaguzi wake wa kupata uongozi mpya uchaguzi ambao utafanyika Disemba 24, 2017.

Matayarisho hayo ya Uchaguzi tayari yameshaanza ambapo zoezi linaloendelea sasa ni kuhakiki Wanachama na kutafuta Wanachama wapya ambapo zoezi hilo lilianza tangu July 2, 2017 na litafikia tamati Agost 15, 2017.

Mwinyimvua Abdi Nzukwi ambae ni Mwenyekiti wa Chama hicho amewaomba Waandishi wa Michezo wa Zanzibar kufanya uhakiki kwa wale ambao ni wanachama na kwa Waandishi wapya wanaotaka kujiunga na chama hicho wajitokeze kwa wingi ili wakachukue fomu za kuomba Uanachama.

“Wanachama wetu tunawaomba wajitokezee kuhakiki taarifa zao mana tunaelekea kwenye Uchaguzi mwishoni mwa mwaka, lakini pia nawaomba Waandishi wa michezo wapya waje kuchukua fomu kujiunga na ZASWA watapata fursa nyingi kama ni waandishi wa michezo hapa Zanzibar, waje kuchukua fomu”. Alisisitiza Nzukwi.
 
Viongozi wa ZASWA, kushoto ni Katibu Donisya Thomas, katikati ni Mwenyekiti Mwinyimvua Abdi na kulia ni Mshika Fedha Mwajuma Juma 


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE