AJIBU AANZA MAKALI YAKE ZENJ, AFANYA VITU SI MCHEZO YEYE NA KAMUSOKO
Kikosi cha Yanga kilichoanza mchezo wa jana |
Mshambuliaji mpya wa Yanga, Ibrahim Ajib jana ameonesha
kiwango cha hali ya juu kabisa katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Mlandege
uliopigwa saa 2 za usiku katika uwanja wa Amaan ambapo Yanga waliibuka na
ushindi wa mabao 2-0.
Mbali ya kuonesha uhodari wake wa kuuchezea mpira Ajibu pia
alifungua akaunti yake ya mabao baada ya kufunga bao lake la kwanza dakika ya
50 katika historia ya klabu yake hiyo mpya tangu ajiunge nayo akitokea Simba.
Bao hilo la Ajib ni msaada mkubwa wa Kiungo wa wakimataifa wa
Zimbabwe Thabani Kamusoko ambae alipiga shuti kali na Ajib akamalizia.
Bao jengine la Yanga lilifungwa na Emanuel Martin dakika ya
73 ambapo ni bao lake la pili katika msimu huu kuanza kufuatia kushinda bao la
ushindi Yanga walipoifunga Singida United 3-2.
Kikosi cha Yanga kimeondoka kisiwani Unguja asubuhi ya leo Jumatatu kwa
Ndege na kwenda Kisiwani Pemba kuweka kambi kujiandaa na pambano na mtani wake,
Simba katika mchezo wa Ngao ya Hisani utakaopigwa Agost 23, 2017 kwenye uwanja
wa Taifa Jijini Dar es salam.
Kikosi cha Mlandege kilichoanza mchezo wa jana |
Big up YANGA SC
ReplyDelete