DALILI KUBWA JKU NA ZIMAMOTO KUWAKILISHA ZANZIBAR MASHINDANO YA CAF BAADA YA BOYS LEO KUFUNGWA NA TAIFA KUSHINDA
Timu ya Jang’ombe boys imekubali kichapo cha bao 1-0
kutoka kwa Okapi katika mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora
uliopigwa jioni ya leo katika uwanja wa Amaan.
Bao pekee la Okapi limefungwa na Seif Saleh dakika ya 66.
Nako huko katika uwanja wa Gombani timu ya Taifa ya Jang’ombe
wakafanikiwa kuichapa Jamhuri mabao 2-0 mchezo uliopigwa leo jioni katika
uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba.
Mabao ya Taifa yote yamefungwa na Ali Badru.
Mpaka sasa JKU anaongoza akiwa na alama 24 akifuatiwa na
Zimamoto mwenye points 22 huku Jamhuri akikamata nafasi ya 3 kwa alama zake 21.
Comments
Post a Comment