DIRISHA LA USAJILI KUFUNGWA KESHO ALHAMIS, HAKUNA KUONGEZA SIKU-KATIBU ZFA
Dirisha la uhamisho na usajili rasmi linafungwa kesho Alhamis
Agost 17 majira ya saa 6:00 za usiku ambapo Makocha na Viongozi wengine wa Vilabu
wamezidi kuwa bize kutafuta wachezaji wanaowahitaji ili kuziboresha timu zao
katika msimu mpya wa mwaka 2017-2018.
Akizungumza na Mtandao huu katibu mkuu wa ZFA Mohd Ali Hilali
“Tedy” amesema usajili unafungwa kesho Agost 17 na wao ZFA hawatoongeza siku
wala muda ukifika wakati uliopangwa zoezi hilo litapigwa kufuli.
“Ni kweli zoezi la uhamisho na usajili linafungwa kesho
Alhamis saa 6:00 za usiku na wala hatutarajii kuongeza siku wala saa, muda
ukifika zoezi hilo litafungiwa”. Alisema Tedy.
Chama cha Soka Visiwani Zanzibar “ZFA” kilitangaza zoezi la
uhamisho na usajili kwa msimu wa mwaka 2017-2018 kufunguliwa July 17, 2017 na
kumaliza kesho Agost 17, 2017.
Zoezi hilo ni kwaajili ya Maraja yote kuanzia ligi kuu soka
ya Zanzibar, ligi daraja la kwanza Taifa, la Pili Taifa hadi ligi za Madara ya
Wilaya.
Duuhhh!!! sawa mkuu tumekuelewa
ReplyDelete