DIRISHA LA USAJILI ZANZIBAR KUFUNGWA LEO ALHAMIS
Dirisha la uhamisho na usajili rasmi litafungwa leo Alhamis
Agost 17 majira ya saa 6:00 za usiku ambapo Makocha na Viongozi wengine wa Vilabu
wamezidi kuwa bize kutafuta wachezaji wanaowahitaji ili kuziboresha timu zao
katika msimu mpya wa mwaka 2017-2018.
Chama cha Soka Visiwani Zanzibar “ZFA” kilitangaza zoezi la
uhamisho na usajili kwa msimu wa mwaka 2017-2018 kufunguliwa July 17, 2017 na
kumaliza leo Alhamis Agost 17, 2017.
Zoezi hilo ni kwaajili ya Madaraja yote kuanzia ligi kuu soka
ya Zanzibar, ligi daraja la kwanza Taifa, la Pili Taifa hadi ligi za Madara ya
Wilaya.
Comments
Post a Comment