JKU YASHINDA 7 YAREJEA KILELENI, HUKU ZIMAMOTO NAE AKIMCHAPA MTU

Timu ya Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU) imefanikiwa kuondoka na kapu la mabao kufuatia kuichapa Kizimbani mabao 7-2 katika mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora uliosukumwa jioni ya leo katika Dimba la Gombani Kisiwani Pemba.

Mabao ya JKU yamefungwa na Khamis Said dakika ya 37, 45,63 Amour Omar dakika ya 19, Muhammed Said Mpopo dakika ya 80,90 na Issa Haidar “Mwalala” dakika ya 89 kwa shuti kali kutoka katikati ya uwanja hadi goli,  huku mabao ya kufutia machozi ya Kizimbani yote yamefungwa na Nassir Suleiman dakika ya 50 na 73.

Mchezo mwengine leo umepigwa katika dimba la Amaan ambapo Zimamoto wakaichapa Mwenge mabao 3-1.

Mabao ya Zimamoto yamefungwa na Ibrahim Hamad Hilika dakika ya 12 na Nyange Othman Denge dakika ya54 na 61 ambapo bao pekee la Mwenge limefungwa na Sharifu Hamad dakika ya 69.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa kupigwa michezo 2 katika viwanja viwili tofauti majira ya saa 10:00 za jioni.


Katika uwanja wa Amaan watasukumana kati ya Jang’ombe boys dhidi ya Okapi na katika uwanja wa Gombani Jamhuri watakipiga na Taifa ya Jang’ombe.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE