JUUKO MURSHID KUTUA ZENJ KUUNGANA NA WENZAKE KAMBI YA SIMBA, NYONI NAE KUTINGA ZENJ KESHO AKITOKEA BURUNDI MSIBANI
Mlinzi wa kati wa Simba Mganda Juuko Murshid wakati wowote
kuanzia leo anatarajiwa kujiunga na wenzake kambini Visiwani Zanziabar kwaajili
ya mazoezi ya kujiandaa na mchezo wao wa Ngao ya Hisani dhidi ya Yanga
utakaupigwa Agost 23, kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salam.
Akizungumza na Mtandao huu Mratibu wa Simba Abbas Suleiman
amesema Juuko yupo Dar es salam akitokea Afrika ya Kusini na leo Jumanne muda
wowote ataungana na wenzake kambi hapa Zanzibar.
“Juuko yupo Dar es salam na muda wowote kuanzia Jumanne ataungana
na wenzake hapa Zanzibar”.
Wakati huo huo mlinzi mpya wa Simba Erasto Edward Nyoni nae
akitarajiwa kuungana na wenzake kuanzia kesho Jumatano ambapo anatokea Burundi
msibani.
“Nyoni ataungana na wenzake kesho Jumatano mana alikuwepo
Burundi kwenye msiba wa bamkwe wake na leo Jumanne atafika Dar es salam kisha
kuja huku Zenj, alikwenda msibani baada ya kufiwa na bamkwe wake hivyo sisi
tulimpa nafasi hiyo na karibu ataungana na wenzake”. Alisema Abbas.
Comments
Post a Comment