KAMBI YA WANAMICHEZO MAJESHI WA TANZANIA YAENDELEA VYEMA VISIWANI ZENJ

Mashindano ya Majeshi ya Michezo ya Afrika Mashariki na Kati mwaka huu yatafanyika Bujumbura Mjini Burundi kuanzia  Agost 20, 2017 ambapo timu za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) litashiriki kwa michezo mitano ikiwemo mpira wa Miguu, mpira wa Kikapu, mpira wa Wavu, mpira wa Pete na Riadha.

Timu hizo za JWTZ zimeweka kambi Visiwani Zanzibar ambapo kambi hiyo inaendelea vizuri mpaka sasa huku wakipania kutwaa ubingwa.

Akizungumza na Mtandao huu Kanal Mwandike ambae ni Mkurugenzi wa Michezo wa JWTZ amesema kambi inaendelea vizuri Zanzibar na  wamepania kufanya kweli mwaka huu.


“Kambi inaendelea vizuri hapa Zanzibar na hakuna tatizo lolote mpaka sasa, tumeshacheza michezo mbali mabli ya kirafiki na timu zinaonesha kiwango cha hali ya juu kabisa, mwaka huu tumepania kufanya vyema kuliko mwaka jana, mana mwaka jana tulishinda nafasi ya pili lakini mwaka huu tutakuwa wa kwanza”. Alisema Kanal Mwandike.




Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE