KAPINGA ATEMBELEA KAMBI YA TIMU YA MAJESHI, AZIDI KUWAPA HAMASA YA KUTWAA UBINGWA

Wanamichezo wa Jeshi la Wananchi Tanzania wametakiwa kuzidisha nidhamu, upendo, umoja na mshikamano katika kuhakikisha wanapata mafanikio katika Mashindano ya Majeshi ya Michezo ya Afrika Mashariki na Kati ya mwaka huu ambayo yatafanyika Bujumbura Mjini Burundi kuanzia Agost 26, 2017.

Wito huo umetolewa na mkuu wa operesheni, mafunzo na michezo ndani ya jeshi la wananchi wa Tanzania Brigidia Jeneral Alfred Kapinga alipotembelea kambi ya timu hiyo ambayo ipo Migombani Jeshini Mjini Unguja.

Alisema nidhamu na upendo ndio silaha kubwa ya mafanikio, hivyo anaamini wakiendelea kutunza watafanikiwa kubeba ubingwa katika mashindano hayo.

“Mulichaguliwa wengi sana lakini mumechujwa na sasa mumebakia nyinyi, naamini nidhamu, upendo, umoja na mshikamano ndio silaha kubwa ya mafanikio yenu, endelezeni naamini mutabeba ubingwa mimi sina wasi wasi na nyinyi”. Alisema Kapinga.


Mashindano ya Majeshi ya Michezo ya Afrika Mashariki na Kati mwaka huu yatafanyika Bujumbura Mjini Burundi kuanzia  Agost 26 ambapo timu za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) litashiriki kwa michezo mitano ikiwemo mpira wa Miguu, mpira wa Kikapu, mpira wa Wavu, mpira wa Pete na Riadha.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS