KOCHA WA JAMHURI MWENYE LESENI A APATA TIMU LIGI KUU BARA

Klabu ya Ruvu Shooting imemteua Abdul mutik Haji (Kiduu) kuwa kocha mpya wa timu yao na kumpa mkataba wa mwaka mmoja, ambapo anaweza akaongezewa miaka mengine akifanya vizuri.

Kiduu mwenye leseni A ya CAF alikuwa Kocha Mkuu wa timu ya Jamhuri ambao ndio vinara wa ligi kuu soka ya Zanzibar na ameondoka hapo Jamhuri baada ya kuagalia maslahi bora ziaidi Ruvu.

Akithibitisha taarifa hizo Kocha Kiduu amesema ni kweli amejiunga na Ruvu na sasa akili yake yote ni kujipanga kuhakikisha timu yake mpya inaleta upinzani mkubwa zaidi katika ligi kuu soka ya Tanzania bara.

“Ni kweli nipo Ruvu na nimefunga mkataba wa mwaka mmoja, kwasasa najipanga kuhakikisha Ruvu inafanya vizuri zaidi ya msimu uliopita katika ligi kuu bara”. Alisema Kiduu.

Kiduu amechukua nafasi ya Malale Hamsini keya ambapo pia alikuwa ni Mzanzibar kufundisha timu hiyo.



Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE