KOMBE LA MTOANO KUANZA RASMI LEO, TIMU 16 ZITASHIRIKI MADARAJA TOFAUTI
MICHUANO ya ligi ya Mtoano inatarajiwa kuanza rasmi leo
Jumatatu kwa kupigwa michezo miwili itakayochezwa saa 8:00 za mchana na saa 10:00
za jioni katika uwanja wa Amaan.
Michuano hiyo ambayo imeandaliwa na ZFA wilaya ya mjini
inashirikisha timu 16 za madaraja tofauti.
Afisa Habari wa chama hicho Mwajuma Juma amesema timu 16
zitashiriki ligi hiyo na mchezo wa kwanza utachezwa saa 8:00 mchana kati ya
Hawai na Urafiki.
Aidha alisema kuwa mchezo mwengine utachezwa saa 10:00 ambao
utawakutanisha timu ya Shaba kutoka kisiwani Pemba dhidi ya African Coast.
Alisema kuwa chama chao kimekuwa na kawaida ya kuandaa
mashindano hayo kila mwaka kwa madhumuni ya kuzipa mazoezi timu ya kujiandaa na
ligi ambapo msimu uliopita Bingwa wa Mashindano hayo timu ya Taifa ya Jang’ombe
ambae msimu huu hakushiriki.
Aidha alizitaja timu nyengine zinazoshiriki ligi hiyo ni pamoja
na Negro United, Gereji, New King, Polisi Bridge, Mwembemakumbi, Raska Zone
City, Kundemba, Elhilal, Black Sailors, Polisi, Ujamaa na Mwembeladu.
Kikosi cha Black Sailors msimu uliopita |
Comments
Post a Comment