KUNA SIRI GANI ZANZIBAR? SIMBA YAWASILI UNGUJA, YANGA YAFIKA PEMBA
Kikosi cha wachezaji 23 cha Simba kimewasili Visiwani
Zanzibar jioni ya leo wakitokea Jijini Dar es salam kwaajili ya kuweka kambi
Mjini Unguja wakijiandaa na mchezo wao wa Ngao ya Hisani dhidi ya Yanga ambao
nao leo asubuhi waliondoka Unguja na kwenda Pemba kwaajili ya kambi pia.
Simba wataweka kambi visiwani hapa mpaka Agost 22, 2017 siku
moja kabla ya mchezo wao utakaopigwa Agost 23 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar
es salam.
Simba watafanya mazoezi kwenye uwanja wa Amaan ambapo
wakitarajiwa kucheza michezo 2 ya kirafiki visiwani hapa.
Kambi ya Simba ipo kwenye Hoteli ya Mtoni Marine iliyopo
Maruhubi Mjini Unguja.
Comments
Post a Comment