LAKIDATU MABINGWA WAPYA KIPWIDA CUP, NABIL JAJA NA ALI BAUSI WAENDELEA KUNGARA
Michuano ya kipwida CUP imefikia tamati jana kwa msimu wa
2017 kwa kupigwa mchezo wa fainal kati ya Njaa kali na Lakidatu ambapo lakidatu
imetwaa ubingwa wa mashindano hayo kwa kutoka na ushindi wa mabao 3-1.
Mchezo huo ambao umehudhuriwa na mashabiki wengi katika dimba
hilo la lion kids huko Maungani Wilaya ya Magharibi B Unguja.
Mabao ya Lakidatu yamefungwa na Nabil Amour “Jaja” dakika ya
3, 31 na Ali Bausi dakika ya 63 na lile la Njaa kali likafungwa na Abrahman
Othman dakika ya 7.
Bingwa ambao ni Lakidatu wamekabidhiwa Ng'ombe, Kombe
kubwa, Medali na seti ya jezi huku
mshindi wa pili timu ya Njaa kali ikapewa medali, seti ya jezi na mbuzi Mnyama
na timu zote shiriki ambazo 16 zimepewa mpira mmoja mmoja.
Safi sana mwanangu NABIL AMOUR JUMA wanakuita JAJA ila kwangu nitaendelea na jina langu la kukuita SHEARER
ReplyDelete