MASHINDANO YA BASEBALL TANZANIA KUFANYIKA KESHO ZANZIBAR
Chama cha Baseball na Softball Zanzibar (ZABSA) kimeandaa
Mashindano maalum ya Mabingwa ya mchezo huo Mashindano ambayo itashirikisha
timu za Zanzibar na Tanzania Bara ambapo kesho Jumamosi yakitarajiwa kuanza na
kumalizika kesho kutwa Jumapili katika viwanja vya Amaan Nje.
Akizungumza na Mtandao huu Mwenyekiti wa Chama hicho Othman
Ali Msabaha amesema lengo la kuandaa Mashindano hayo ni kuzidi kuuhamasisha
mchezo huo ambao kwa Zanzibar una miaka 3 wakati kwa bara una miaka 8 tangu
kuanzishwa kwake.
“Lengo la Mashindano haya ni kuzidi kuusambaza huu mchezo
mana tunataka uzidi kukuwa kwa kasi sana, na pia tunataka uwe mpaka kwenye
vikosi vya ulinzi na mitaani isiwe kwenye Mashule tu”. Alisema Msabaha.
Jumla ya timu 4 zitashiriki Mashindano hayo zikiwemo mbili
kutoka Tanzania Bara timu ya Skuli ya Azania pamoja na Kibasila ambapo kwa
Zanzibar zitashiriki timu za Skuli ya Mwanakwerekwe pamoja na Kombain ya
Unguja.
Comments
Post a Comment