NUSU FAINALI MAJIMBO CUP KUANZA KESHO JUMAMOSI

Mashindano ya Majimbo ya Unguja hatua ya Nusu fainali itapigwa kesho Jumamosi Agost 5, 2017 kati ya Jimbo la Mji Mkoongwe dhidi ya Afisi kuu ya CCM Kisiwandui saa 10:00 za jioni katika uwanja wa Amaan.

Kwa mujibu wa mratibu wa Mashindano hayo Uledi Said amesema mechi hiyo itakuwa bila ya kiingilio.

“Matayarisho yamekamilika mechi nusu ya kwanza itachezwa Jumamosi nay a pili Jumapili na hakuna kiingilio”. Alisema Uledi.

Nusu fainali ya pili itapigwa Jumapili Agost 6, 2017 kati ya Jimbo la Kwahani dhidi ya Kikwajuni saa 10:00 za jioni katika uwanja wa Amaan.


Bingwa wa Mashindano hayo atazawadiwa gari aina ya Carry.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE