RAIS WA MASHABIKI WA MTIBWA AWATOA HOFU WENZAKE


Rais wa Mashabiki wa Mtibwa Sugar ya Mkoani Morogoro Suleiman Nassoro “Super Cicinho” amewataka mashabiki wenzake wasiwe na hofu na timu yao katika msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara kwani wamepandisha wachezaji wanne wapya kutoka timu yao ndogo wenye vipaji vya hali ya juu.

Amesema licha ya timu yao kuondokewa na nyota kadhaa waliyokimbilia Simba na timu nyengine lakini bado anaamini watafanya vizuri katika msimu mpya na kuleta upinzani mkubwa kwenye ligi hiyo.

“Hatuna wasi wasi wowote licha ya kuondoka nyota wetu ambao waliokuwa tegemeo, Mtibwa ni chuo tumeshapandisha wachezaji wengine wanne wapya ambao wanauwezo mkubwa na watakuwa tegemeo kwetu na Taifa kwa ujumla”.

Nyota hao wanne waliyopandishwa ni washambuliaji Ismail Aidan na Omary Sultan pamoja na walinzi Dickison Job na Jamal Masenga.


Agost 28, 2017 Mtibwa Sugar wataanza kucheza mchezo wao wa kwanza wa ligi kuu soka Tanzania bara kwenye uwanja wao wa Manungu Morogoro dhidi ya Stand United ya Shinyanga mchezo utakaopigwa saa 10:00 za jioni.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE