SIMBA YABANWA NA MLANDEGE, KESHO WATAKIPIGA TENA NA GULION
Kikosi cha Simba |
Timu ya wekundu wa Msimbazi Simba jana imebanwa mbavu na
watoto wa Abdul Satar timu ya Mlandege baada ya kutoka sare tasa 0-0 kwenye
mchezo wa kirafiki uliopigwa katika uwanja wa Amaan saa 2 za usiku.
Simba iliwachezesha nyota wake kadhaa wapya akiwemo Mlinda
Mlango Aishi Manula, mlinzi Salim Mbonde pamoja na kiungo Haruna Niyonzima huku
washambuliaji wake wapya hatari Emmanuel Okwi pamoja na John Bocco hawakucheza.
Huu ni mchezo wa kwanza kwa timu ya Simba kucheza Visiwani
hapa ndani ya msimu huu mpya ambapo pia ni mchezo wake wa tano wa kirafiki katika
kipindi hichi cha kujiandaa na msimu mpya wa mwaka 2017-2018.
Simba walicheza mechi mbili walipokwenda Afrika ya Kusini
kuweka kambi ambapo walifungwa 1-0 Orlando Pirate, kisha wakatoka sare ya 1-1
na Bidvest baada ya hapo wakaichapa Rayon Sport ya Rwanda 1-0 kwenye mchezo wa
siku ya Simba uliopigwa uwanja wa Taifa Dar es salam kisha kuwafunga Mtibwa
Sugar 1-0 na jana kutoka sare ya 0-0 na Mlandege.
Kwa upande wa Mlandege Jumapili iliyopita ya Agost 13
walichapwa 2-0 na Yanga kwenye uwanja huo huo wa Amaan ambapo jana wakatoka
sare ya 0-0 na Simba.
Simba watashuka tena dimbani kesho Jumamosi Agost 19, 2017
saa 2:00 za usiku katika uwanja wa Amaan ambapo watacheza na timu ya Gulioni FC
“Chama la Wana na Upendo”.
vp waheshimiwa mbona hamna habar mpya kulikoni ?
ReplyDelete