TAIFA YA JANGOMBE YAIPIGA NEGRO KWENYE MCHEZO WA KUTEST MITAMBO
Timu ya Taifa ya Jangombe (Wakombozi wa Ngambo) wamefanikiwa
kutoka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Negro FC katika tamasha la Negro day
mchezo uliopigwa jana usiku katika uwanja wa Amaan.
Mabao ya Taifa yamefungwa na Said Kipara pamoja na Abdallah
Mudhihir “Mido”.
Aidha katika mchezo huo timu zote zilipata fursa ya
kuwatambulisha wachezaji wao wapya waliowasajili katika msimu mpya wa mwaka
2017-2018 ambapo Taifa watashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar wakati Negro
watacheza ligi daraja la pili taifa.
Comments
Post a Comment