UJAMAA NA UKONGWE WAO WAFUNDISHWA SOKA NA VIJANA WA GULIONI
Kikosi cha Ujamaa Sports Club |
Timu kongwe Visiwani Zanzibar Ujamaa Sports Club wamekubali
kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa vijana wa Gulion FC kwenye mchezo maalum wa
Sherehe za kutimiza miaka 60 kwa Ujamaa mchezo ambao umesukumwa jana saa 2 za
usiku kwenye uwanja wa Amaan.
Mabao ya Gulioni katika mchezo huo yamefungwa na Abdul Hamid
Ramadhan dakika ya 45, Ali Juma dakika ya 71 na Shaabani Hassan dakika ya 88
huku bao pekee la Ujamaa likifungwa na Mwinyi Ame dakika ya 79.
Ujamaa ndio timu aliyewahi kucheza kwa kiwango cha hali ya
juu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ambapo
Katika mchezo huo Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari Utalii Utamaduni na
Michezo Zanzibar Mh Rashid Ali Juma akimuwakilisha Makamu wa Pili wa Rais
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ambae pia alikuwa mlinda mlango hatari wa timu
hiyo miaka iliyopita.
Msimu huu mpya wa mwaka 2017-2018 Ujamaa itashiriki ligi
daraja la Pili Taifa Unguja wakati Gulioni FC itacheza ligi daraja la Pili
Wilaya ya Mjini.
Kikosi cha Gulioni FC |
Comments
Post a Comment