YANGA SC YAFIKA UNGUJA LEO USIKU KUCHEZA NA MLANDEGE, KESHO ASUBUHI PEMBA KWAJILI YA MPAMBANO WAO DHIDI YA SIMBA
MABINGWA wa soka wa Tanzania Bara, Yanga wamewasili kisiwani
Unguja leo saa 5 za asubuhi wakitokea Jijini Dar es salam ambapo leo saa 2:00
za usiku watacheza mchezo wa kirafiki na Mlandege SC mchezo ambao utapigwa
katika uwanja wa Amaan.
Yanga wamefikia katika Hoteli ya Lail-Noor ambayo ipo Maisara
Mjini Unguja.
Kesho asubuhi Yanga wataondoka kisiwani Unguja na kwenda
Kisiwani Pemba kuweka kambi kujiandaa na pambano na mtani wake, Simba katika
mchezo wa Ngao ya Hisani utakaopigwa Agost 23, 2017 kwenye uwanja wa Taifa
Jijini Dar es salam.
Comments
Post a Comment