ZIMAMOTO NA JAMHURI, BOYS ZAGOMBEA NAFASI YA KUSHIRIKI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA, WAPISHANA KWA POINT 1 NA UMEBAKI MCHEZO 1
Kikosi cha Zimamoto |
Bingwa mpya wa ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu wa mwaka
2016-2017 tayari ameshapatikana ambae ni JKU huku akiwa amebakiwa mchezo mmoja
mkononi dhidi ya Mwenge utakaopigwa Jumamosi ya Agost 19, 2017 katika uwanja wa
Amaan.
Lakini homa kali katika ligi hiyo ni nani atamaliza nafasi ya
pili kati ya Zimamoto yenye alama 25 au Jamhuri yenye points 24 au Jangombe Boys yenye alama 24 pia ambapo wote
wamebakiwa na mchezo mmoja mkononi.
Kwa mujibu wa ratiba Zimamoto atamalizana na Kizimbani wakati
Jamhuri watakipiga na Jang’ombe Boys ambapo michezo hiyo ilikuwa imepangwa siku
tofauti katika uwanja wa Gombani yani Jumamosi na Jumapili lakini kutokana na umuhimu
wa michezo hiyo ZFA huenda ikalazimika michezo hiyo kuipanga siku moja na
wakati mmoja ili kuepusha upangaji wa matokeo.
Bingwa na Makamo Bingwa wa ligi hiyo watawakilisha Zanzibar
katika Mashindano ya Kombe la Klabu Bingwa pamoja na Kombe la Shirikisho Barani
Afrika ambapo msimu uliopita waliwakilisha Zimamoto na KVZ ambao wote
walitolewa mzunguko wa kwanza.
Comments
Post a Comment