ZIMAMOTO YAUNGANA NA JKU KUWAKILISHA ZANZIBAR CAF
Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka ya Zanzibar timu ya
Zimamoto imefanikiwa kumaliza ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora kwa
kushika nafasi ya pili baada ya kuichapa Kizimbani mabao 8-1 mchezo uliopigwa
jana katika uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba.
Kwa matokeo hayo Zimamoto imefikisha alama 28 na kushika
nafasi ya pili ambapo Bingwa wa ligi hiyo ni JKU alitangazwa karibu ya wiki
moja nyuma.
Bingwa (JKU) na Makamo Bingwa wa ligi hiyo (Zimamoto)
watawakilisha Zanzibar katika Mashindano ya Kombe la Klabu Bingwa pamoja na
Kombe la Shirikisho Barani Afrika ambapo msimu uliopita waliwakilisha Zimamoto
na KVZ ambao wote walitolewa mzunguko wa kwanza.
Comments
Post a Comment